Mwakilishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Josephine Lyengi akitoa mada katika kikao kazi cha kujadili hali halisi ya haki za binadamu nchini na kuibua matukio ambayo bado yanaonekana ni changamoto kubwa na kuyatengenezea mpango kazi wa kushughulikia. Kikao hicho kinafanyika Mkoani Morogoro kuanzia Oktoba 24—25, 2019.
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imekutanisha makundi ya haki za binadamu iliyoyaunda ili kujadili hali ya haki za binadamu na kuibua matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu kwenye makundi ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu ili kuandalia mpango kazi wa kwenda kuyashughulikia.