Kaimu Katibu Mtendaji, Hajjat Fatuma Muya (katikati) akiongea katika warsha ya kupeana mrejesho wa kazi za robo mwaka (Julai-Septemba) iliyofanyika kwa siku tatu (3), kuanzia Oktoba 21—23, 2019 Mkoani Morogoro. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Umma, Mawasiliano, Utafiti na Nyaraka kutoka Tume, Alexander Hassan, na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi kitengo cha Mipango kutoka Tume, Laurent Burilo.
Marehemu Getrude Alex pichani enzi za uhai wake
Wakili Clarence Kipobota akisisitiza jambo katika kikao kazi cha siku tatu cha kupeana mrejesho wa kazi walizofanya kati ya Tume na AZAKI na kuandaa taarifa ya pamoja ya robo mwaka ya hali ya haki za binadamu nchini kilichofanyika Mkoani Morogoro, Oktoba 21—23, 2019.
Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mette N. Dissing-Spandet akiongea na Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu katika mazungumzo yaliyofanyika kwenye ofisi za THBUB jijini Dar es Salaam mwishoni mwa juma.
Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Pontian Kitorobombo akiongea katika mkutano wa baraza la Wafanyakazi la THBUB
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Ndugai akiongea na viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hawapo pichani) walipotembelea ofisini kwake Wilayani Kongwa Novemba 19, 2019. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume, Mheshimiwa Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa , Deogratius Ndejembi.