ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

THBUB ya waasa Watendaji Kata na Vijiji kuzingatia utawala bora

17 Jan, 2025
THBUB ya waasa Watendaji Kata na Vijiji kuzingatia utawala bora

Watendaji wa Kata na Vijiji wahimizwa kutenda haki na kuzingatia misingi ya utawala bora katika utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo ameyabainisha Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala   Bora(THBUB) Mhe. Mohamed Khamis Hamad wakati akitoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo kuhusu haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa  Watendaji hao ,yaliyofanyika 
Januari 16,2024 katika Ukumbi wa Isawima, Wilaya ya Kaliua ,Mkoani Tabora.

Mhe. Mohamed alisema kuwa  Watendaji wa Kata na Kijiji ni daraja la kuunganisha Serikali na Wananchi ili kuinua maendeleao kwa pamoja hivyo Watendaji hao wanapaswa kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi kwa kuzingatia sheria zilizoekwa ili kusimamia  na misingi ya utawala bora utakaosaidia kuleta maendeleo katika Jamii.

Pia Mhe.Mohamed alieleza kuwa kumekuwa na malalamiko katika baadhi ya maeneo kuwa  Watendaji kutokuwashirikisha wananchi  ikiwemo kuwasomea taarifa ya mapato na matumizi ya Kata na Kijiji ili kuimarisha msingi wa uwazi na kuondoa sintofahamu kwa wananchi kuhusu matumizi ya fedha za maendeleo.

“Kumekuwa na changamoto nyingi katika maeneo mbalimbali yanayohusiana na wananchi kutopewa taarifa ya mapato na matumizi ya Kijiji ,kwani kufanya hivyo ni kuwanyima haki na kukiuka misingi ya utawala bora” alisema Mhe. Mohamed

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Kaliua Bw. Raymond Mweli amewataka Watendaji hao kutenda haki kwa Jamii pamoja na kuwaelimisha juu ya haki na wajibu wao.

“Mafunzo mtakayopata mtumie kama njia  ya kuongeza ufanisi na uadilifu kwenu na Jamii kwa ujumla”alisema Bw. Mweli


Katika Ziara hiyo THBUB imetoa mafunzo ya haki za binadamu na misingi ya utawala pamoja na kuzindua Klabu ya Haki za Binadamu katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii na Shule ya Sekondari Kaliua

Aidha,THBUB imefanya mkutano wa hadhara na kupokea kero  mbalimbali za wananchi wa Kata  ya Ufukutwa