ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

Kitengo cha Ununuzi na Ugavi

i. Kushauri uongozi kuhusu masuala yanayohusu ununuzi wa bidhaa na huduma pamoja na usimamizi wa vifaa;

ii. Kuhakikisha kuwa Tume inazingatia taratibu na miongozo ya ununuzi kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma;

iii. Kutekeleza na kufuatilia mpango wa mwaka wa ununuzi wa Tume;

iv. Kununua, kutunza na kusimamia vifaa, bidhaa na huduma ili kusaidia mahitaji ya vifaa ya Tume;

v. Kuhakikisha utunzaji sahihi na uhifadhi wa vifaa, usambazaji wa vifaa na mahitaji ya ofisi kwa wakati na kwa kiwango cha kutosha;

vi. Kutunza na kusasisha orodha ya bidhaa, vifaa na mahitaji ya ofisi; na

vii. Kutoa huduma za Katibu kwa Bodi ya Zabuni kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma.