ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

Majukumu ya Tume

Majukumu ya Tume

Kazi za Tume zinatekelezwa kulingana na dira, dhima na malengo ya Tume kama

zilivyoainishwa katika Ibara ya 130 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka

1977 na katika kifungu cha 6 (1) vifungu vidogo (a) mpaka (o) vya Sheria ya Tume. Majukumu

hayo ni kama ifuatavyo:

Kukuza nchini kinga na hifadhi ya haki za binadamu na wajibu kwa jamii kwa mujibu

wa Katiba na Sheria za nchi;

b) Kupokea malalamiko ya uvunjwaji wa haki za binadamu kwa ujumla;

c) Kufanya uchunguzi juu ya mambo yanayohusu uvunjaji wa haki za binadamu na

ukiukwaji wa misingi ya utawala bora ;

d) Kufanya utafiti katika, kutoa na kueneza nchini elimu kwa umma kuhusu haki za

binadamu na utawala bora;

e) Inapobidi, kufungua mashauri mahakamani yanayolenga kukomesha ukiukwaji wa

haki za binadamu au kurekebisha haki zinapovunjwa au misingi ya utawala bora

inapokiukwa;

f) Kuchunguza mwenendo wa mtu yeyote au taasisi yoyote ambayo vifungu vya

sehemu hii vinahusiana navyo katika utaratibu wa kawaida wa kutekeleza kazi za

ofisi yake au utendaji wa kazi unaokiuka mamlaka yake;

g) Kupeleleza au kuchunguza malalamiko yanayohusiana na utekelezaji au utendaji wa

watu wanaoshikilia ofisi katika utumishi wa Serikali, mamlaka za umma au vyombo

vya umma, ikijumuisha taasisi binafsi na watu binafsi ambapo malalamiko hayo

yanadaiwa kuwa ni ya matumizi mabaya ya madaraka, huduma za upendeleo kwa

mtu yeyote, ikiwa ni mlalamikaji au mtu mwingine, katika kutekeleza kazi zao za

kiserikali au umma;

h) Kutembelea Magereza na mahala pengine wanamozuiliwa watu au sehemu

zinazofanana kwa madhumuni ya kutathmini na kukagua hali za watu wanaozuiliwa

sehemu hizo na kutoa mapendekezo yatakayowezesha kurekebisha kasoro zilizopo

kwa mujibu wa matakwa ya Sheria hii;

i) Kuchukua hatua za kusaidia kusahihisha, kurekebisha, kuzuia au kukomesha vitendo

vilivyotajwa katika vifungu (e), (f), (g) au (h) kutokana na njia za usawa sahihi na

haki, ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za kisheria;

j) Kutoa ushauri kwa Serikali na kwa vyombo vingine vya umma na taasisi za sekta

binafsi juu ya mambo maalum yanayohusiana na haki za binadamu na utawala bora;

k) Kutoa mapendekezo yanayohusiana na sheria iliyokwishatungwa au inayokusudiwa

kutungwa, kanuni, au mambo ya kiutawala ili kuhakikisha zinakubaliana na haki za

binadamu na za misingi ya utawala bora;

l) Kusaidia uridhiaji wa au utiaji saini mikataba au makubaliano yanayohusu haki za

binadamu, kuzilinganisha sheria za nchi na kufuatilia na kutathmini utekelezaji ndani

ya Jamhuri ya Muungano na Serikali na watu wengine, kwa viwango vya haki za

22

binadamu vilivyoainishwa kwenye mikataba au makubaliano au chini ya sheria za

kawaida za mahusiano ya kimataifa ambayo Jamhuri ya Muungano inawajibika nayo

m) Kwa kupitia Serikali, kushirikiana na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa

Nchi za Afrika, Jumuia ya Madola na taasisi nyingine zenye uhusiano baina yao,

miongoni mwao au ya kikanda na taasisi za nchi za nje ambazo zina uzoefu katika

ulinzi na ukuzaji wa haki za binadamu na utawala bora;

n) Kuchukua hatua zifaazo kwa ajili ya ukuzaji na uendelezaji wa upatanishi na

usuluhishi miongoni mwa taasisi na watu mbalimbali ambao hufika au hufikishwa

mbele ya Tume;

o) Kufanya kazi nyinginezo zozote kama zinavyoweza kuelezwa katika sheria nyingine.

Aidha, ibara ya 131 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeainisha maeneo

ambayo Tume haina mamlaka kuyachunguza kama ifuatavyo.

a) Jambo lolote ambalo liko mbele ya Mahakama au chombo kinginecho cha

Kimahakama.

b) Jambo lolote linalohusu uhusiano au mashirikiano kati ya Serikali ya nchi yoyote ya

nje au shirika la Kimataifa

c) Jambo linalohusu madaraka ya Rais kutoa msamaha.

d) Jambo jingine lolote lililotajwa na sheria yoyote.