ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

KLABU YA HAKI ZA BINADAMU SHULE YA SEKONDARI  MWANDIGA KUWAJENGEA UWEZO WANAFUNZI WENZAO

16 Feb, 2025
KLABU YA HAKI ZA BINADAMU SHULE YA SEKONDARI  MWANDIGA KUWAJENGEA UWEZO WANAFUNZI WENZAO

Ujumbe wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora THBUB ukiongozwa na Kamishna Mhe. Amina Talib Ali  umezindua klabu ya haki za binadamu Shule ya Sekondari ya  Mwandiga iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma DC leo 13 Februari 2025.

Uzinduzi wa klabu hiyo umefanyika wakati Ujumbe huo ulipofika Shuleni hapo kwa lengo la kutoa elimu ya kusimamia na kulinda 
haki za binadamu na uelewa wa Misingi ya Utawala Bora na kuitaka klabu hiyo kuwa balozi wa kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi wenzao. 

Aidha Ujumbe wa THBUB umetoa elimu kwa Wanafunzi hao namna ya kupinga na kutoa taarifa ya vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa vikitokea katika jamii mbalimbali