ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

THBUB  KUSHIRIKIANA  NA MAMLAKA YA KUDHIBITI  DAWA ZA KULEVYA.

09 Jul, 2025
THBUB  KUSHIRIKIANA  NA MAMLAKA YA KUDHIBITI  DAWA ZA KULEVYA.


Katika kumlinda mtoto na kuandaa jamii bora ya sasa na baadae ipo haja  ya mashirikiano baina ya Tume ya Haki za Binadamu  na Mamlaka ya Kudhibiti dawa za Kulevya.

Hayo amesemaKamishna  wa THBUB  mhe Amina Tali Ali wakati akizungumza  na Kamshna Generali wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya  alipotembelea banda la THBUB  katika Maonesho ya  Kimataifa  ya Biashara  "Sabasaba"Jijini Dar es Salaam Julai 5,2025


Mhe.Amina amesema kuwa watoto wengi wa sasa uingia katika makundi mabaya na kujihusisha na kutumia dawa za kulevya ,ambapo upelekea kupoteza haki zao za msingi.

"Kushirikiana kwa THBUB  na DCEA itasaidia katika kuleta watoto hawa katika mstari"amesema mhe. Amina

Kwa upande wake Kamishna Generali wa Mamlaka ya Kudhibiti  Dawa za Kulevya Bw.Aretas Lyimo amesema kuwa  ushirikiano utasaidia kupunguza au kupoteza kabisa matumizi ya dawa za kulevya kwakuwa watoto  watakua wamepata elimu ya haki za binadamu ,ambayo wakitumia dawa za kulevye wanapoteza haki zao"


 Bw Lyimo amebainisha haki mbalimbali  ambazo mtoto anaeza kupoteza anapotumia dawa za kulevye ikiwemo haki ya kuishi,haki ya afya na elimu na  nyingine "


Aidha Bw.ameomba THBUB  kushirikiana kwa pamoja kupitia Klabi za  haki za binadamu za   ili kujenga kutoa elimu ambayo inawasaidia  watoto kutambua madahara ya dawa za kulevya na kupata haki zao