ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

THBUBYAPOKEA MAlALAMIKO ZAIDI YA 2923 YA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA  BORA.

09 Jul, 2025
THBUBYAPOKEA MAlALAMIKO ZAIDI YA 2923 YA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA  BORA.


Miongoni  mwa majukumu ambayo THBUB  inayotekeleza  ni kupokea Malalamiko  ya Wananchi  yanayohusu ukiukwaji wa haki za binadamu  na misingi ya utawala  bora
Hayo amesema Kamishna Tume ya Haki za Binadamu  na Utawala Bora Mhe.Amina Talib Ali wakati  akizungumza  na waandishi  wa habari alipotembelea banda la THBUB  katika Maonesho ya Kitaifa ya Biashara Julai 4,2025 Jijini Dar es Salaam.


Mhe.Amina  amesema kuwa malalamiko  ya uvunjifu wa haki za binadamu  bado yapo na katika kipindi cha miaka minne jumla ya malalamiko 2923 yamepokelewa na THBUB  ambayo tunaendelea kuyashughulikia
"Malalamiko hayo sio lazima alalamikiwe kiongozi hata mtumishi ambaye amepewa jukumu lakutekeleza asipofanya hivyo anakiuka misingi ya utawala bora” mesema mhe.amina


 Pia.Mhe.Amina ametaja malalmiko yalilopokelewa zaidi katika kipindi  hicho ni kuhusu ardhi na mifuko ya hifadhi ya Jamii
"THBUB  tunapokea malalamiko mengi  ya wastaafu kupata kiinua mgongo  ambacho hakutarajia  au kutopata haki kwa wakati ,changamoto hii inatokana taasisi aliokua anafanyia kazi haifikishi michango kwa wakati lakini THBUB  inasaidia  mtu huyo apate haki yake "amesema mhe.Amina

Mhe.Amina ametaja changamoto mbalimbali ya ushughulikiaji wa malalamiko hayo ikiwemo kwa baadhi ya Taasisi zinzolalamikiwa kutokuwa na ushirikiano pindi THBUB inapopeleka  taarifa ya kulalamikiwa
"THBUB inapokea na kupeleka kuwasilisha malalamiko  kwa mlalamikiwa ,THBUB  inaandika barua lakin hayajibiwi kwa wakati na kuna muda haijibiwi kabisa "
Nitoe  wito kwa viongozi   wa taasisi tunapowandikia barua,watujibu kwa wakati ili tuweze kuwajibu walalamikaji kwa wakati ili wapate haki zao