VIJANA WAASWA KULINDA AMANI NCHINI

Katika kudumisha na kuimarisha amani ya nchi, vijana waaswa kuwa mstari wa mbele kuilinda.
Wito huu umetolewa na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Mhe. Amina Talib Ali wakati wa kuadhimisha Siku ya Sheria iliyoandaliwa na Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dodoma iliyofanyika Aprili 25, 2025 katika Ukumbi wa CIVE Auditorium ulipo chuoni hapo. Mada ya Kongamano hilo ilikuwa ni “Nafasi ya Kliniki za Sheria za Vyuo Vikuu katika kuhakikisha Uchaguzi Huru, Haki na Uwazi Tanzania”
Mhe. Amina Talib Ali amesema kuwa amani ni kitu kikubwa sana nchini kabla na baada ya uchaguzi tuhakikishe kuwa maandalizi yote ya uchaguzi yanafanyika kwa amani bila kuleta machafuko.
“Ni wajibu kila mwananchi kuhakikisha kwamba tunakwenda kwenye uchaguzi kukiwa na amani’
Pia, Mhe. Amina amesema kuwa miongoni mwa haki zilizoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 ni uhuru wa kutoa maoni na haki ya kushiriki katika shughuli za uongozi ikiwemo kuchagua au kuchaguliwa.
“Hivyo kila mmoja wetu ajue kwamba anayo haki ya kushiriki katika masuala ya uchaguzi lakini hakikisha unafuata Sheria, miongozo na taratibu zilizowekwa’ amesema Mhe. Amina.
Kwa hatua nyingine Mhe. Amina ameupongeza Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kuchagua mada hiyo ambayo imeenda sambamba ikiwa tunaelekea katika uchaguzi mkuu mwaka huu