ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

VIJANA WAASWA KULINDA AMANI NCHINI

28 Apr, 2025
VIJANA WAASWA KULINDA AMANI NCHINI

Akizungumza wakati wa kuadhimisha Siku ya Sheria  Chuo Kikuu cha Dodoma iliyofanyika Aprili 25,2025 katika Ukumbi wa CIVE Auditorium ulipo chuoni hapo Kamishna Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe.Amina Talib Ali amesema kuwa amani ni kitu kikubwa sana nchini kabla na baada ya uchaguzi tuhakikishe kuwa maandalizi yote ya uchaguzi yanafanyika kwa amani bila kuleta machafuko.

“ Ni wajibu kila mwananchi mmoja kuhakikisha kwamba tunakwenda kwenye uchaguzi kukiwa na amani’

Pia Mhe Amina  amesema kuwa miongoni mwa haki zilizotaja katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni haki ya kutoa maoni ikiwemo haki hii ya kupiga kura 
“ hivyo kila mmoja ajue kwamba anayo haki ya kupiga kura lakini hakikisha unafuata sheria, miongozo na taratibu zilizopo’ amesema Mhe.amina 


Mhe.Amina ameupongeza Uongozi  wa Chuo Kikuu cha Dodoma kwakuchagua Mada ya ”Nafasi ya Kliniki za Sheria za Vyuo Vikuu  katika kuhakikisha Uchaguzi Huru,Haki  na Uwazi Tanzania”mada hii imeenda sambamba  ikiwa tunaelekea katika uchaguzi mkuu mwaka huu