ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAO KULINDA HAKI ZA BINADAMU

22 Sep, 2025
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAO KULINDA HAKI ZA BINADAMU


Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imetoa wito kwa  waandishi wa habari kote nchini kuzingatia 
maadili ya taaluma yao katika kuhabarisha Umma  katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu Octoba 2025 ili kulinda haki za binadamu.

Wito huo umetolewa na Makamu mwenyekiti THBUB Mhe. Mohamed Khamis Hamad alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya kwa waandishi wa habari yaliyolenga kuwajengea uwezo kuhusu haki za binadamu na wajibu wa waandishi wa habari.

Mafunzo hayo yamefanyikia katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jijini Arusha Septemba 17, 2025.

Mhe. Hamad wamewakumbusha waandishi wa habari  kuwa wana wajibu wa kuripoti habari zao kwa usahihi, kwa uwiano  na bila upendeleo kwa chama au mgombea yeyote.

 Aidha, amewataka kuepuka matumizi ya lugha ya matusi, kejeli, udhalilishaji, pamoja na kuchapisha au kutangaza taarifa  zenye viashiria vya uchochezi, hasa kupitia mitandao ya kijamii.

“Vyombo vya habari ni kiungo muhimu kati ya wananchi, wagombea na taasisi za uchaguzi, hivyo vinapaswa kuwa chanzo cha taarifa sahihi na si chombo cha kueneza taarifa za uongo na potofu. Maadili ya uandishi, uhuru wa habari na ulinzi wa haki za binadamu ni nguzo muhimu zinazopaswa kupewa kipaumbele na kila mwanahabari wakati wa utekelezaji wa majukumu yake amesema Mhe. Hamad.

Aidha,  aliongeza kuwa, THBUB inatarajia  waandishi wa habari watatekeleza majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia sheria, hivyo kuchangia uchaguzi wa amani, haki na huru.