ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

WANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU VIZURI KUDUMISHA MSHIKAMANO NA AMANI- THBUB

22 Sep, 2025
WANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU VIZURI KUDUMISHA MSHIKAMANO NA AMANI- THBUB

 

Tume huru  ya haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB )imewataka waandishi wa habari mkoani Tabora kufuata miiko na kanuni za uandishi wa habari kwa kuzingatia usawa, kuepuka matumizi mabaya ya lugha ili kudumisha mshikamano na amani hususani kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika  Oktoba 29,2025.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi msaidizi  elimu kwa Umma na Mawasiliano kutoka THBUB , Zawadi Msalla ,wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa  mkoa wa Tabora juu  namna bora ya kutoa taarifa zao .

"Waandishi wa habari tumieni kalamu zenu vizuri  ili kuijenga Tanzania yenye mshikamano ,ili kuweza hata kufanya Tanzania iwe kati ya nchi zinazohesabika  kama kisiwa cha amani" Zawadi alisema .

Bi. Zawadi , ameongezea kuwa  waandishi wa habari wanayo nguvu kubwa kuijenga nchi yenye mshikamano na amani kupitia taarifa wanazo toa  hivyo hawana budi kuzingatia misingi na weledi katika kazi zao.

Kwa upande wao, baadhi ya waandishi wa habari akiwemo Lubango Mleka , Maiko George na Said Kapalila , wamesema mafunzo hayo yamewaimalisha katika namna bora ya kuripoti kwa weledi na kwa kuzingatia misingi ya uandishi wa habari hususani kuelekea uchaguzi mkuu