THBUB, THRDC wakutana kuzungumzia mashirikiano
26 Jan, 2021
Asubuhi ya leo maafisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG); Bi. Beatrice Beda (kushoto) pamoja na Bw. Mbaraka Kambona (kulia), wametembelea ofisi za Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) na kufanya mazungumzo na Afisa Uwezeshaji wa THRDC Wakili Deo Bwire (katikati) juu ya jinsi gani CHRAGG na THRDC wanaweza kuboresha ushirikiano katika kufanya kazi za Utetezi wa Haki za Binadamu nchini kwa ukaribu zaidi katika siku za usoni. Huu ni mwendelezo mzuri wa mahusiano ya muda mrefu kati ya CHRAGG na THRDC, lakini pia ni mwanzo mzuri kwa Tume ya Haki