ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

MFUMO WA PAMOJA KUWEZESHA TAASISI KUWASILIANA

23 Jun, 2025
MFUMO WA PAMOJA KUWEZESHA TAASISI KUWASILIANA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  amezitaka taasisi za umma ambazo hazijajiunga na mfumo wa pamoja unaowezesha mifumo mbalimbali ya serikali kuwasiliana na kubadilishana taarifa(Government Enterprise Services Bus-GoVesb) kuhakikisha kuwa zimejiunga katika mfumo huo kabla  au ifikapo Juni 30, 2025 

Hayo ameyasema Waziri Mkuu,  Mhe.Majaaliwa Kassim Majaaliwa (Mb) wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Viwanja vya Chinangali Park Dodoma Juni 23, 2025.

Mhe.Waziri amesema kuwa  mfumo huu utasaidia  kuboresha huduma zinazotolewa na serikali.

Sambamba na hilo, Mhe Majaaliwa amewataka watumishi kushiriki uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, 2025 kwa kuwa kuchagua ama kuchaguliwa ni haki ya msingi ya kikatiba.

"Tumieni haki hii"amesema Mhe.Majaaliwa

Maadhimisho  ya Wiki ya Utumishi  wa Umma yalifunguliwa 16,2025 na kuhitimishwa Juni23,2025.
Aidha Tume ya Haki za Binadamu  na Utawala Bora ni moja kati ya Taasisi 143 zilizoshiriki kutoa huduma katika Maadhimisho  hayo