ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

Idara ya Elimu kwa Umma, utafiti na Nyaraka

Majukumu ya Divisheni

i.Kuishauri Tume kuhusu masuala ya elimu kwa umma na mawasiliano;

ii. Kuandaa na kusambaza  machapisho ya elimu kuhusu haki za binadamu, wajibu wa raia na huduma zitolewazo na Tume;

iii. Kufanya tafiti kuhusu hali ya haki zabinadamu na utawala bora nchini;

iv. Kusimamia Kituo cha Haki za Binadamu na Utawala Bora cha Nyaraka na Taarifa;

 v. Kufanya uchambuzi  na tathmini ya kimfumo kuhusu masuala ya haki za binadamu na utawala bora;

vi. Kuandaa miongozo ya  utekelezaji wa majukumu ya Idara; na
vii. Kuandaa taarifa za kila mwaka, za vipindi maalum na  za dharura kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Tume pamoja na hali ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora.