MTUMISHI AJIRA MPYA AAPISHWA KUWA MTUMISHI WA THBUB
28 May, 2025

Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Dkt. Thomas Masanja, amemuapisha Mtumishi Mpya Bw. Bryan B. Kimario kuwa Mtumishi wa THBUB katika kada ya Uhasibu Daraja II.
Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za THBUB Makao Makuu, Mtaa wa Kilimani, Dodoma, Mei 27, 2025.
Wakati wa uapisho huo, Kamishna Dkt. Masanja amesisitiza umuhimu wa kuzingatia taratibu za kazi, akimhimiza Kimario kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu, ufanisi na kujituma, kwa manufaa ya taasisi na jamii kwa ujumla.