ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

WANAFUNZI  UVINZA WAPATIWA ELIMU YA HAKI ZA BINADAMU. 

10 May, 2026
WANAFUNZI  UVINZA WAPATIWA ELIMU YA HAKI ZA BINADAMU. 

Utoaji wa elimu ya haki za binadamu  na utawala bora katika maeneo ya shule umelenga kujenga uelewa kwa wanafunzi kutambua haki na wajibu wao.

Hayo yameelezwa na  Afisa Uchunguzi  Tume ya Haki za  Binadamu na Utawala Bora, Bw. Raphael Mavunde wakati akitoa elimu ya haki za binadamu  na utawala  bora  Mei 07, 2026 katika shule za sekondari za Mazungwe na Ruchugi zilizopo Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma.

Bw. Mavunde amesema kuwa utoaji wa elimu ya haki za binadamu  na utawala bora katika maeneo ya  shule ni kwaajili ya kujenga uelewa  kwa wanafunzi kuweza kutambua haki  na wajibu wao. "Utoaji wa elimu hii itasaidia kujenga jamii inayojua haki za binadamu", amesema Bw. Mavunde.

Pia wanafunzi wameelezwa  kuwa utawala bora ni utawala  unaozingatia sheria, uwajibikaji na  usawa. "Ninyi tunategemea mtakuwa  viongozi  wa baadae, ni wajibu  kutambua kuwa kiongozi bora ni yule anaezingatia haki za binadamu  na misingi ya utawala bora" amesema Bw. Mavunde

Naye mwalimu Grace Kinabo amewashukuru maafisa wa THBUB kwa kutoa elimu hiyo ambayo itakua na manufaa kwa sasa na baadae.

slot gacor