ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

SKAUT DODOMA  WAPATIWA  ELIMU  YA HAKI  ZA BINADAMU  NA UTAWALA  BORA.

10 Aug, 2026
SKAUT DODOMA  WAPATIWA  ELIMU  YA HAKI  ZA BINADAMU  NA UTAWALA  BORA.

 

Wanachama wa Skauti Dodoma wamepatiwa elimu ya haki za binadamu  na utawala bora walipotembelea banda la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB)  kwenye Maonesho  ya Wakulima Nanenane  yanayofanyika Viwanja vya John Malecela, Nzuguni Jijini Dodoma.

Wanachama hao walipatiwa elimu kuhusu haki  mbalimbali zikiwemo haki ya kuishi, usawa mbele ya sheria, elimu, afya, kumiliki mali, uhuru wa kutoa maoni na elimu kuhusu misingi  ya  utawala bora. 

Akitaja baadhi ya misingi ya utawala bora, Kaimu Mkurugenzi sehemu ya Utafiti na Nyaraka THBUB, Bw. Paul Sulle alisema misingi hiyo imewekwa ili kuhakikisha jamii inaishi katika amani na haki.

"Uwazi , ushirikishwaji, usawa mbele ya sheria na uwajibikaji ni miongoni mwa  nguzo  muhimu za misingi  ya utawala bora" amesema Bw. Sulle.

Akizungumza  kwa niaba ya wanachama hao Godfrey  Elia ameishauri THBUB  kuwa na mkakati wa kutoa elimu kwa wanachama wa Skauti  nchi nzima ili kuwaongezea uelewa  zaidi wa masuala ya haki za binadamu na utawala bora.

slot gacor