ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

Muundo wa Tume

 

Tume inaundwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Makamishna watano (5) na Makamishna Wasaidizi ambao idadi yao haikutajwa kwenye Sheria. Wote huteuliwa na Rais kutokana na mapendekezo ya Kamati ya Uteuzi ambayo inapokea maoni kutoka kwa wananchi.Wajumbe wa Tume ni watu walio na uzoefu na taaluma mbalimbali. Hufanya kazi kwa kipindi cha miaka mitatu, na wanaweza kuteuliwa kwa kipindi cha pili kisichozidi miaka mitatu. Chini ya Tume kuna Sekretarieti, ambayo inawajibika kwa kazi za siku hadi siku. Katibu Mtendaji ndiye anayeongoza Sekretarieti na anawajibika kwa Tume kuhusiana na masuala ya kiutawala na utekelezaji wa majukumu ya Tume kama taasisi ya usimamiaji wa haki.

Muundo wa Sekretarieti

Utendaji kazi wa Tume umegawanywa katika Idara, kila moja inaongozwa na Mkurugenzi, na kila Idara imegawanywa katika seksheni chini ya Wakuu wa seksheni.

Idara hizo ni zifuatazo:

1. Divisheni  ya Malalamiko na Uchunguzi

2. Divisheni ya Elimu kwa Umma, Mawasiliano, Utafitina Nyaraka

3. Divisheni  ya Huduma za Kisheria

4. Divisheni  ya Utawala na Rasilimali Watu.

 

Aidha, kuna vitengo vifuatavyo katika Tume:

Kitengo cha Fedha na Uhasibu;
Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani;
Kitengo cha Mipango na Bajeti;
Kitengo cha Usimamizi wa manunuzi;
Kitengo cha TEHAMA;
Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini;

Kitengo cha Haki Jinai
Ofisi ya Zanzibar na
Ofisi za Matawi (Dar es salaam, Mwanza, Mtwara  Pemba, na  Tabora ambayo imeanzishwa mwezi Juni, 2025 )