Muundo wa Tume
Tume inaundwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Makamishna watano (5) na Makamishna Wasaidizi ambao idadi yao haikutajwa kwenye Sheria. Wote huteuliwa na Rais kutokana na mapendekezo ya Kamati ya Uteuzi ambayo inapokea maoni kutoka kwa wananchi.Wajumbe wa Tume ni watu walio na uzoefu na taaluma mbalimbali. Hufanya kazi kwa kipindi cha miaka mitatu, na wanaweza kuteuliwa kwa kipindi cha pili kisichozidi miaka mitatu. Chini ya Tume kuna Sekretarieti, ambayo inawajibika kwa kazi za siku hadi siku. Katibu Mtendaji ndiye anayeongoza Sekretarieti na anawajibika kwa Tume kuhusiana na masuala ya kiutawala na utekelezaji wa majukumu ya Tume kama taasisi ya usimamiaji wa haki.
Muundo wa Sekretarieti
Utendaji kazi wa Tume umegawanywa katika Idara, kila moja inaongozwa na Mkurugenzi, na kila Idara imegawanywa katika seksheni chini ya Wakuu wa seksheni.
Idara hizo ni zifuatazo:
1. Divisheni ya Malalamiko na Uchunguzi
2. Divisheni ya Elimu kwa Umma, Mawasiliano, Utafitina Nyaraka
3. Divisheni ya Huduma za Kisheria
4. Divisheni ya Utawala na Rasilimali Watu.
Aidha, kuna vitengo vifuatavyo katika Tume:
Kitengo cha Fedha na Uhasibu;
Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani;
Kitengo cha Mipango na Bajeti;
Kitengo cha Usimamizi wa manunuzi;
Kitengo cha TEHAMA;
Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini;
Kitengo cha Haki Jinai
Ofisi ya Zanzibar na
Ofisi za Matawi (Dar es salaam, Mwanza, Mtwara Pemba, na Tabora ambayo imeanzishwa mwezi Juni, 2025 )